Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Taasisi ya Elimu Tanzania

Mkurugenzi Mkuu
Dkt. Aneth Komba
Mkurugenzi Mkuu

Kuhusu TET

Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) ni taasisi ya Umma iliyo chini ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia (WyEST) iliyoanzishwa chini ya Sheria ya Bunge Na. 13 ya Mwaka 1975 (Marejeo ya 2002). Kuanzia mwaka 2009, TET ilifanywa kuwa Taasisi ya Elimu ya Juu isiyokuwa Chuo Kikuu kupitia usajili wa Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTVET) wenye namba REG/040. Taasisi ina jukumu la kutafsiri kwa vitendo Sera za Serikali kuhusu Elimu kwa kubuni mitaala na Programu za elimu zitakazowezesha utoaji wa elimu bora katika ngazi ya Elimu ya Awali, Msingi, Sekondari na Elimu ya Ualimu. Majukumu mahsusi ya TET  NI: Kubuni, kuandaa na kuboresha Mitaala  kwa ngazi za Elimu ya Awali, Msingi, Sekondari na Vyuo vya Ualimu; Kuandaa vifaa saidizi vya kutekeleza mtaala na kuhakiki ubora wa vifaa vinavyolengwa kutumiwa katika ngazi zilizo chini ya mamlaka yake; Kutoa  mafunzo kwa watekelezaji na wasimamizi wa Mitaala; na Kufanya Utafiti na kutoa ushauri wa kitaalamu katika masuala ya mitaala, ufundishaji na ujifunzaji  na elimu kwa ujumla.

service
Uuzaji na Usambazaji wa Vitabu
service
Huduma za kumbi za mikutano
service
Darasa Janja
service
Uthibiti Ubora
Miaka 50 ya Taasisi ya Elimu Tanzania