Viwanda vya Uchapishaji
Viwanda vya Uchapishaji
Taasisi ya Elimu Tanzanaia (TET) ina viwanda vya uchapaji vilivyopo Dar es Salaam, Mbeya, Mwanza na Morogoro, . Viwanda hivyo hutoa huduma za kuchapisha vitabu, vipeperushi, kalenda, shajara (diary), hotuba za wizara, mitihani ya shule, mafaili ya kutunzia kumbukumbu za ofisi, vitambulisho vya kazi, na kazi nyingine za uchapaji. TET inawakaribisha wadau wa elimu kutoka sekta ya umma na binafsi na watanzania wote kupata huduma bora za uchapaji kwa gharama nafuu toka katika viwanda vya TET. Kwa maelezo zaidi kuhusu huduma zinazotolewa na gharama za huduma hizo, wasiliana na Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Uchapaji kupitia 0764158891.