Wizara ya Elimu ,Sayansi na Teknolojia na Tume ya Mipango zajadili Rasimu ya Sera na Mitaala.
Imewekwa: 07th September, 2023
Tarehe 06/09/2023 Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknolojia na Tume ya Mipango zimefanya kikao cha pamoja cha majadiliano ya muelekeo wa sekta ya elimu nchini kwa kuzingatia rasimu ya Sera na Mitaala zilizofanyiwa maboresho.
Kikao hicho cha majadiliano kimefanyika jijini Dar es salaam kilichoongozwa na Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Tekonolojia, Dkt.Carolyne Nombo na kwa upande wa Tume ya Mipango alikuwa ni Katibu Mtendaji Lawrence Mafuru.
Katika kikao hicho Mwenyekiti wa Kamati za Sera ya Elimu na Mafunzo, Prof.Joseph Semboja na Mwenyekiti wa Kamati ya Kitaifa ya Maboresho ya Mitaala, Prof.Makenya Maboko kwa pamoja waliwasilisha mapitio ya Sera ya Elimu na Mitaala.
Wengine waliohudhuria kikao hicho ni pamoja na wajumbe wa kamati hizo na Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Elimu Tanzania(TET) Dkt. Aneth Komba akiwa na wataalamu kutoka TET.