MAFUNZO YA MTAALA ULIOBORESHWA KWA WALIMU WAKUU
MAFUNZO YA MTAALA ULIOBORESHWA KWA WALIMU WAKUU
Imewekwa: 12 August, 2024

Moja kati ya walimu wakuu akiwasilisha mtazamo kutoka kwenye kikundi chake wakati mafunzo ya Mtaala ulioboreshwa yakiendelea Mkoani Kilimanjaro
Mafunzo ya Mtaala ulioboreshwa kwa walimu wakuu wa shule za msingi za Serikali na zisizo za Serikali yanaendelea katika Mkoani Kilimanjaro lengo ni kuongeza ufanisi katika usimamiaji wa utekelezaji wa Mtaala huo nchini. Mafunzo hayo ya siku mbili yameanza Juni 11, 2024 ambapo yanaendeshwa na Waratibu kutoka Taasisi ya Elimu Tanzania kwa kushirikiana na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia pamoja pamoja pamoja na OR TAMISEMI. Mafunzo hayo yanaendelea katika vituo mbalimbali nchi nzima ambapo walimu wanapata fursa ya kufahamu Mtaala huo kiundani na mbinu mbalimbali za kuutekeleza ili ulete tija kwa taifa.