MAFUNZO KWA NJIA YA DARASA JANJA
MAFUNZO KWA NJIA YA DARASA JANJA
Imewekwa: 20 January, 2025

Taasisi ya Elimu Tanzania inaendelea kutoa mafunzo ya Mtaala ulioboreshwa kwa walimu wa kidato cha kwanza shule ya sekondari Nahukahuka, wilaya ya Mtama, mkoa wa Lindi kupitia darasa janja (s
Taasisi ya Elimu Tanzania inaendelea kutoa mafunzo ya Mtaala ulioboreshwa kwa walimu wa kidato cha kwanza shule ya sekondari Nahukahuka, wilaya ya Mtama, mkoa wa Lindi kupitia darasa janja (smart class).
Mafunzo hayo ya siku tatu yameanza leo Januari 6, 2025, lengo ni kuujua Mtaala huo na kuwapitisha walimu katika mbinu mbalimbali za kuutekeleza ili kuendelea kuleta matokeo chanya katika taifa.